Thursday, December 17, 2009

 

Haki za Wanyama


Hata wanyama wana haki zao na zinastahili kuheshimiwa. Basi hili la abiria jijini Dar es salaam (daladala) ambalo hutoa huduma kati ya Gongo la Mboto na Mwenge limebeba mbuzi ambaye amefungwa juu kana kwamba ni mzigo. Hata nyama inaweza kuwa tamu kweli!

Tuesday, December 08, 2009

 

JK akijibu tu, mipasho itakuwa ruksa





Pichani Rais Kikwete akifafanua jambo wakati akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kuwasili jijini Dar es salaam akitokea ziara ndefu iliyohusisha bara la Amerika Kaskazini na visiwa vya Carribea. Kushoto na makamu wa rais, Dk Shein


Rais Jakaya Kikwete jana alirejea nchini akitokea kwenye ziara ndefu iliyomchukua kwenye nchi kadhaa duniani. Alianzia Jamaica akashuka Trinidad na Tobago kabla ya kwenda Cuba ambako alielezea jinsi alivyomuhusudu Che Guevera na baadaye kusogea Marekani kwa uchunguzi wa afya.
Lakini shangwe za mapokezi ziliambatana na maswali juu ya yale aliyoyaacha yakijiri hapa nchini, na hasa ule mdahalo ulioandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere ambao ulibua maswali mengi juu ya utendaji wa mkuu huyu wa nchi.
Si kawaida kwa watu, hasa wanaotoka kwenye chama kimoja kuhoji utendaji wa kiongozi wao, lakini mawaziri wa zamani, Matheo Qares, Mussa Nkangaa na katibu mkuu wa CCM wa zamani, Phillip Mangula walieleza hofu yao juu ya utendaji wa rais na mwenyekiti wao wa chama. Na Qares alidiriki kusema kama mheshimiwa hataweza kuchukua maamuzi magumu kabla ya 2010, basi CCM haina budi kutafuta mgombea mwingine wa kiti hicho.
Nkangaa, ambaye pia aliwahi kuwa mbunge mkoani Singida, alieleza kuwa chama kimepoteza hadhi yake na sasa kimesahau wafanyakazi na wakulima na kukumbatia matajiri. Mangula alishangazwa na jinsi chama kinavyoendeshwa kwa sasa.
JK alikumbana na maswali kuhusu masuala hayo yote na kwanza akadokeza kuwa hashangazwi na hao waliosema hayo, lakini pili akatoa neno ambalo limenitia shaka kidogo kwamba atakaa na wenzake - bila ya shaka akina Nkangaa, Qares, Mangula, Salim na Warioba si wenzakew- na kujiandaa kujibu hayo makombora.
Ndipo hapo napojiuliza kama kuna umuhimu kwa JK kujibu maoni ya hao waliokosoa utendaji au kufanya kazi nzuri ili iwe majibu tosha kwa wote wenye mashaka naye.
Nadhani JK akithubutu na kuanza kujibu hayo, atakuwa amefungua jukwaa kubwa la mipasho ambalo halitakuwa na msimamizi maana hata rais na mwenyekiti wa chama tawala atakuwa amejitumbukiza katika kushambuliana.
Ndio maana nasubiri kwamba akijibu tu, basi mipasho itakuwa ruksa

 



Jamaa akiimba kile kibao maarufu cha Greatest Love of All huku akisindikizwa na jamaa kibao - labda wengine wako mtungi wakati wa sherehe ya End of the Year za MCL.

 

Ahly, Zamalek ni kufa na kupona leo





Na Mwandishi Wetu
MACHO ya mashabiki wa soka ambao daima huvutiwa zaidi na upinzani wa klabu zinazotoka mji mmoja, leo yataelekezwa Cairo nchini Misri ambako Al Ahly itakuwa ikipambana na Zamalek katika mechi ya daby ambayo inachukuliwa kuwa ina vurugu kubwa kuliko nyingine zote duniani.
Mechi hiyo baina ya timu za jijini Cairo itakuwa ya pili baina ya vigogo hao msimu huu baada ya kushindwa kufungana katika mechi ya kwanza iliyochezeshwa na mwamuzi kutoka Ubelgiji, Frank de Bleeckere.

Mbelgiji huyo atapuliza filimbi tena leo wakati Al Ahly, klabu yenye mafanikio kuliko zote barani Afrika, itakapovaana na wapinzani wao wakubwa wa jijini Cairo.

Kwa sasa Ahly inaongoza msimamo wa ligi kwa tofautin ya pointi tano, ikifuatiwa na Ismailia na ndiyo inayopewa nafasi zaidi ya kuibuka kidedea dhidi ya Zamalek, ambayo imepoteza mechi tatu zilizopita na ambayo iko juu kidogo ya timu zilizo hatarini kushuka.
Kocha mpya wa Zamalek, Hossam Hassan ana wasiwasi na wachezaji wake ambao wana majeraha, hasa mshambuliaji hatari Amr Zaki ambaye anauguza nyonga, wakati Hossam Arafat na Sayed Mosaad hawataweza kucheza mechi hiyo. Kuna mashaka na hali ya Alaa Ali ambaye anaughua mafua.
Upinzani baina ya timu hizo mbili umekuwa wa muda mrefu kiasi kwamba umehamia hadi nje ya uwanja, ukisababisha vifo, uvunjaji wa nyumba na wakati fulani ligi nzima kufutwa.
Vurugu za mashabiki zilisababisha serikali ya Misri kupiga marufuku mechi baina ya klabu kutoka jiji moja kutumia uwanja wa klabu moja na hivyo mechi za wababe hao wawili sasa zinachezwa kwenye uwanja mmoja tu wa Cairo International Stadium.
Upinzani wao umefikia kiwango kwamba hata waamuzi wa Misri hawaaminiki na Chama cha Soka cha Misri sasa kinalazimika kutumia marefa kutoka barani Ulaya ili kuondoa upendeleo.
Mwamuzi mkongwe Kenny Clark, ambaye aliwahi kuchezesha mechi nne za Old Firm, yaani baina ya vigogo wa Glasgow nchini Scotland, Celtic na Rangers, aliteuliwa kuchezesha mechi ya watani hao mwaka 2001 baada ya vyama sita vya soka barani Ulaya kukataa kutuma waamuzi wake.
Kabla ya hapo, mechi iliyochezeshwa na mwamuzi wa Ufaransa Mark Batta, ilivunjika baada ya wachezaji wa Zamalek kugoma kuendelea na mchezo wakipinga mchezaji wao, Ayman Abdel Aziz kuonyeshwa kadi nyekundu katika dakika yab pili kwa kukwatua kwa nyuma.
Asili ya upinzani baina ya timu hizo unasemekana kuanzia nyakati ambazo majeshi ya Uingereza yalikuwa kwenye mitaa ya jiji la Cairo. Wakati huo, mpira wa miguu ulikuwa ukichukuliwa kama utamaduni pekee uliojipenyeza kwenye nchi ya Misri, lakini iliichukua nchi hiyo miaka kadhaa hadi 1907 ilipoanzisha klabu ya kwanza ya soka, Al Ahly, iliyokuwa ikiendeshwa na wenyeji.
Ikapewa jina la Al Ahly kumaanisha Taifa na rangi zake zikawa nyekundu ya zamani ambayo ilikuwa ikitumika kabla ya wakoloni wa Kiingereza kuvamia nchi hiyo. Al Ahly ikawa ikichukuliwa kama klabu kwa ajili ya taifa hilo, ikikutanisha watu wa kada mbalimbali na matabaka mbalimbali.
Zamalek, ambayo huvalia rangi nyeupe, ilikuwa ikichukuliwa kama klkabu ya nje na ya watui wa nje. Pia ilikuwa klabu ya mfalme ambaye alikuwa akichukiwa, King Farouk. Awali klabu hiyo ilipewa jina la mfalme huyo, lakini ikabadilishwa na kuitwa Zamalek baada ya mfalme huyo kuondolewa.
Mwanzoni timu hiyo ilikuwa na mashabiki ambao ni Waingereza na watu wa nje ambao hawakupenda mwenendo mpya wa utaifa wa Misri. Kwa hiyo upande mmoja ukawa wa rangi nyekundu yab watu maskini na wanaojivunia utaifa wao wakati upande mwingine ukawa wa matajiri, wa daraja la kati na wanaotaka mabadiliko.
Makundi hayo yapo hadi leo.
Klabu hizo mbili si bora nchini Misri tu, bali Afrika nzima huku Al Ahly ikiwa imetangazwa kuwa klabu bora ya karne na Shirikisho la Soka Afrika (CAF).

 

Mangula auchambua
uongozi wa Kikwete

Sadick Mtulya
UTAWALA wa Rais Jakaya Kikwete umezidi kukosolewa baada ya katibu mkuu wa zamani wa CCM, Philip Mangula kuuchambua, akisema unasumbuliwa na mambo matatu makubwa, ikiwa ni pamoja na kupeana uongozi kwa urafiki.
Mangula anaendeleza mjadala wa siku za karibuni ambao umekuwa shubiri kwa CCM, ambayo imelazimika kutoa kauli kadhaa kujibu mashambulizi dhidi ya mwenyekiti wake.
Makada wa mwisho kuikosoa serikali ya Kikwete walikuwa mawaziri wa zamani, Matheo Qares na Juma Nkangaa ambao walieleza wasiwasi wao kama mkuu huyo wa nchi ana uwezo wa kufanya maamuzi magumu na kwamba CCM imepoteza mwelekeo kwa kuamua kukumbatia wafanyabiashara na kuachana na sera yake ya kuwa chama cha wakulima na wafanyakazi.

Safari hii, Mangula ambaye alikuwa mtendaji Mkuu wa CCM kabla ya kuteuliwa kwa Makamba, ameibuka na kueleza udhaifu wa chama hicho tawala na kikongwe barani Afrika na ambacho hakuna shaka kwamba kinapitia kwenye wakati mgumu kwa sasa.

Mangula ambaye alihudhuria kongamano la Mwalimu Nyerere jijini Dares Salaam ambalo liliibua hoja nyingi dhidi yab serikali ya Kikwete wiki iliyopita, hakuchangia maonin yake katikam mjadala huo, lakini
baadaye alifanya mahojiano na Mwananchi na kutaka mambo matatu ambayo yanautafuna uongozi wa Rais Kikwete.

Mangula alitaja mambo hayo kuwa ni ubinafsi, kufanya maamuzi kabla ya kuelimisha wananchi na kuwepo kwa wigo finyu wa majadiliano na wadau katika masuala mbalimbali.

Mangula, ambaye alishika nafasi ya katibu mkuu wa CCM kwa kipindi cha miaka kumi ya uongozi wa serikali ya awamu ya tatu, alitahadharisha kuwa iwapo mambo hayo hayatarekebishwa kwa haraka na kwa kipaumbele kinachostahili, taifa litaelekea pabaya zaidi.

“Utawala wa sasa umetofautiana na tawala nyingine kwa kupungukiwa na mambo matatu ya msingi ambayo ni ubinafsi, kufanyika maamuzi kabla ya kuelimisha wananchi pamoja na kutokuwepo kwa wigo mpana wa majadiliano kuhusu masuala mbalimbali ya mustakabali wa taifa,” alisema| Mangula.

Mangula alisema hali hiyo imesababishwa na watu wengi wanaopewa uongozi kutokuwa sifa za kuongoza na kwamba wamepata nafasi hizo kwa njia za urafiki.

“Hata utaratibu mzima wa kuwapata viongozi wanaostahili kwa sifa haupo, badala yake mambo yanafanywa kwa urafiki,” alisema Mangula ambaye amekuwa kimya kwa muda mrefu.

Akifafanua hoja zake hizo, Mangula alisema katika utawala wa sasa ubinafsi ndio umeonekana kuchukua kipaumbele katika kutatua mambo muhimu ya kitaifa.

Mangula aliweka bayana kwamba katika utawala uliopita ubinafsi haukupewa nafasi kwa kuwa kabla kiongozi hajazungumzia jambo lolote, alilazimika kupata mawazo ya chama tawala na wanachama kuhusu anachotaka kuzungumza.

Aliongeza kwamba kutotumika kwa mfumo huo ndio sababu ya kupishana kwa kauli za viongozi kunakoendelea kutamba kwenye safu za mbele za vyombo vya habari kwa sasa.

“Tabia ya kutaka kuonekana kuwa wewe ni bora kuliko mwingine ipo, ndio maana leo viongozi, tena wa kutoka chama kimoja, wanapishana kauli kuhusu jambo moja,” alifafanua.

Akizungumzia kufanyika kwa maamuzi kabla ya kuwaelimisha wananchi, Mangula alisema hilo ni tatizo linaloendelea kulalamikiwa na Watanzania.

Mangula alisema katika utawala uliopita watu walielimishwa kwanza kabla ya kufikiwa kwa maamuzi.
“Utaratibu wa kuelimisha kwanza kabla ya kufikiwa kwa maamuzi ndio uliokuwa ukitumika, lakini hali sasa inaonekana kuwa tofauti,” aliongeza.

Kuhusu kutokuwepo kwa wigo mpana wa majadiliano katika masuala ya kitaifa, Mangula alisema hiyo inatokana na viongozi wachache waliopewa dhamana na wananchi kuamini kuwa mawazo yao yanajitosheleza.

Hoja za Mangula, ambaye kwa sasa anajishughulisha na masuala ya kilimo, zinashabihiana na zile zilizowahi kutolewa na mawaziri wakuu wawili wastaafu, Dk Salim Ahmed Salim na Jaji Joseph Warioba kuhusu mustakabali wa taifa.

Jaji Warioba alinukuliwa na vyombo vya habari hivi karibuni akitahadharisha kuwa nchi inaelekea kubaya kutokana na mambo mbalimbali kuendeshwa kinyume.

Warioba, ambaye alishika nafasi hiyo ya mtendaji mkuu wa serikali kwenye miaka ya themanini, alifafanua kuwa taifa linakabiliwa na matatizo mengi ikiwemo ukosefu wa maadili ya uongozi, rushwa na hata utaratibu mzima wa kuendesha mambo na kubainisha kuwa kuna pengo kubwa katika kuaminika kwa serikali.

Naye Dk Salim Hamed Salim, ambaye aliwahi kuwa katibu mkuu wa Umoja wa Afrika (OAU), alisema mfumo wa serikali ya Tanzania kwa sasa umeoza kwa rushwa na hivyo hauwezi kumsaidia rais kuikabili, hivyo rushwa kutawala kuliko kitu kingine.

Dk Salim alisema wakati wa utawala wa awamu ya kwanza wa Mwalimu Julius Nyerere, rushwa ilidhibitiwa kikamilifu, lakini wakati huu rushwa imeachiwa nafasi kubwa na kufanya hali ya Watanzania idorore.

Alisema tofauti kubwa kati ya awamu hizo na ile ya Mwalimu Nyerere ni kuwa muasisi huyo wa taifa alionyesha kwa vitendo kuwa rushwa ni jambo aliloamua kulifungia mkanda na kupambana nalo, lakini baada ya hapo tatizo hilo limeachiwa liendelee kiasi cha rushwa kugeuka kuwa utaratibu.

Mwanadiplomasia huyo aliongeza kwamba, licha ya nia njema ya Rais Kikwete ya kupambana na rushwa na ufisadi, bado mfumo mzima wa serikali umeoza kiasi ambacho haiwezekani kupambana na rushwa.

Baadaye wakati wa kongamano lililoandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Qares, ambaye alikuwa Waziri wa Menejimenti ya UItumishi wa Umma katika serikali ya awamu ya tatu, na Nkangaa ambaye alikuwa waziri katika serikali ya awamub ya pili, waliibuka.

Qares alimtaka Rais Kikwete awe jasiri na kufanya maamuzi magumu na akashauri kuwa akishindwa kufanya hivyo hadi 2010, CCM isimpitishe kugombea urais 2010.

Qares, ambaye pia aliwahi kuwa mkuu wa mkoa wakati wa uongozi wa Benjamin Mkapa, alisema Rais anapaswa kufumba macho na kuwashughulikia hata wale wanaosema hakukutana nao barabarani.

Naye Nkangaa alisema CCM imepoteza heshima yake na kubaki kuwa chama cha matajiri wachache na kutupa mkono wakulima na wafanyakazi, ndiyo maana inasuasua kuwachukulia hatua watuhumiwa katika kashfa za Kagoda na Richmond.

Tangu kutolewa kwa ripoti ya kashfa ya utoaji zabuni ya uzalishaji umeme wa dharura kwa kampuni ya Richmond, wabunge wa CCM wamekuwa wakitofautiana sana katika hoja, baadhi wakiunga mkono kujiuzulu kwa Edward Lowassa katika nafasi ya uwaziri mkuu na kutaka hatuia zaidi zichukuliwe, huku wengine wakipinga.
Hali ilizidi kuwa mbaya katika mkutano uliopita wakati wabunge walipoicharukia serikali yao wakiituhumu kufanya mambo kwa ubinafsi na kubariki mikataba mibovu, na mjadala huo uliilazimisha CCM kuitisha mkutano wake wa Halmashauri Kuu.
Lakini mkutano huo ukawa moto mbaya zaidi baada ya Spika Samuel Sitta kunusurika kuvuliwa uanachama kutokana na kundi linalotuhumiwa kwa ufisadi kujipanga vyema kushughulikia wanaowatuhumu.
Mijadala mikali kwenye kikao cha Halmashauri Kuu iliisha kwa CCM kuunda kamati ya wazee wa busara, ikilongozwa na rais wa serikalinyab awamu ya tatu, Ali Hassan Mwinyi ambayo mwezi uliopita ilisababisha kizaazaa kingine wakati ilipoongea na wabunge kuhusu kudhoofika kwa mahusiano baina ya wanachama na viongozi wa chama hicho tawala.
Lakini mkutano huo ukawa jukwaa zuri kwa watuhumiwa wa ufisadi kujibu mashambulizi yanayotolewa kila mara hadharani dhidi yao na hasa kwenye vikao vya Bunge.
Katika mikutano hiyo ya Kamati ya Mwinyi, makamanda wa vita dhidi ya ufisadi walijikuta wakibebeshwa tuhuma nzito na kutolewa maneno machafu, kiasi kwamba hali ndani ya CCM ikaonekana kuwa si shwari na haikuwa ajabu wakati mawaziri hao wa zamani pamoja na Mangula kujitokeza na kuuchambua utawala wa Kikwete kuwa una matatizo.

Friday, November 27, 2009

 

Sita wateuliwa kusimamia uchaguzi Yanga

Sosthenes Nyoni

UONGOZI wa klabu ya Yanga umetangaza majina ya wajumbe watano watakaounda kamati itakayosimamia uchaguzi mkuu wa klabu hiyo uliopangwa kufanyika Januari 3 mwakani.

Mwenyekiti wa Yanga, Imani Madega alisema kuwa kamati hiyo itafanya kazin kwa kushirikiana na Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Soka Tanzania(TFF).

Madega aliwataja watu wanaunda kamati hiyo kuwa ni pamoja na Jaji John Mkwawa ambaye atakuwa mwenyekiti wa kamati hiyo, Ridhiwan Kikwete ambaye ni mtoto wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Angetile Osiah , Philemon Ntahilaja na mwenyekiti wa zamani wa matawi ya Yanga asili, Yusuph Mzimba.

Alisema kuwa uteuzi huo umezingatia katiba ya klabu hiyo iliyofanyiwa marekebisho Agosti 8 2006 iliyotaka kamati ya uchaguzi kuwa na watu wasiopungua watano na wasiozidi saba.

"Uteuzi wa majina haya umezingatia katiba ya Yanga iliyofanyiwa marekebisho Agosti 8 2006 ambapo inaelekeza kuwa kamati ya uchaguzi inatakiwa kuwa na watu wasiopungua watano na wasiozidi saba,"alisema Madega.

Aliongeza kuwa uongozi wa klabu hiyo utakutana na wajumbe hao ili kuelezana majukumu yanayotakiwa kufanywa wakati wa zoezi hiyo la uchaguzi.

Madega, pia aliwataka wanachama wa klabu hiyo kutumia haki yao ya kuwachagua viongozi wanaowataka kwa kuhakikisha wanalipa ada za uanachama wao ili wawe wanachama hai na wenye sifa za kushiriki uchaguzi.

"Haki mojawapo ya mwanachama ni kuchagua kiongozi anayemtaka, hivyo natoa wito kwa wanachama ambao hawajamaliza ada za uanachama wao walipe ili wawe na sifa ya kushiriki katika uchaguzi,"alisema Madega.

Thursday, November 26, 2009

 
CAF reminds National Associations of Inter-clubs entry deadline
11-25-2009
CAF reminds National Associations of  Inter-clubs entry deadline
Zoom
The Confederation of African Football is reminding all National Associations to submit the list of their representatives for the CAF Inter-clubs competitions, Orange CAF Champions league and Orange Confederation Cup, before 30th of November 2009.
According to Article 2, paragraph 2 of CAF Inter-clubs regulations, the application must reach CAF by mail, fax or e-mail not later than 30th of November of the year preceding the Competition.

 

Tanzanian Striker Joseph Kaniki Signs for Swedish Premier Side

Former Tanzanian Simba striker Joseph Kaniki has finally signed a two-year contract with Gefle IF of Sweden for the Premier Division League.

Ndumbalo Soccer Agency managing director Damas Ndumbalo told The Citizen that striker passed his trials in Sweden. Kaniki will join fellow Tanzanian Haruna Moshi who secured a contract with the Swedish club recently.

"The duo flew to Sweden for trials with Gefle earlier this month and both have passed their trials," he said.

Kaniki, who was plying his trades at Rayon Sports of Rwanda, finished his contract before moving to Sweden. Ndumbaro said they had already applied for his International Transfer Certificate (ITC) from Rwanda's soccer body, FERWAFA.

Simba allowed Moshi to fly out to Sweden only three days before clashing with their archrivals, Young Africans in the high flier Dar Es Salaam.


 

Ratiba ya fainali za Kombe la Dunia 2010

Pilikapilika za Kombe la Dunia ndio zimeshaanza na hii hapa ni ratiba ya fainali hizo kabla ya kuchomekwa majina ya nchi.

Ijumaa, Juni 11

Kundi A

Team 1 v Team 2, Johannesburg (Soccer City)

Team 3 v Team 4, Cape Town

Saturday, June 12

Kundi B

1 v 2, Johannesburg (Ellis Park)

3 v 4, Port Elizabeth

Group C

1 v 2, Rustenburg

Jumapili, Juni 13

Kundi C

3 v 4, Polokwane

Group D

1 v 2, Durban

3 v 4, Pretoria

Jumatatu, Juni 14

Kundi E

1 v 2, Soccer City

3 v 4, Bloemfontein

Group F

1 v 2, Cape Town

Jumanne, Juni 15

Group F

3 v 4, Rustenburg

Kundi G

3 v 4, Port Elizabeth

1 v 2, Ellis Park

Jumatano, Juni 16

Kundi H

3 v 4, Nelspruit

1 v 2, Durban

Group A

1 v 3, Pretoria

Alhamisi, Juni 17

Kundi A

4 v 2, Polokwane

Group B

4 v 2, Bloemfontein

1 v 3, Soccer City

Ijumaa, Juni 18

Kundi D

1 v 3, Port Elizabeth

Kundi C

4 v 2, Ellis Park

1 v 3, Cape Town

Jumamosi, Juni 19

Kundi D

4 v 2, Rustenburg

Kundi E

1 v 3, Durban

4 v 2, Pretoria

Jumapili, Juni 20

Kundi F

4 v 2, Bloemfontein

1 v 3, Nelspruit

Kundi G

1 v 3, Soccer City

Jumatatu, Juni 21

Kundi G

4 v 2, Cape Town

Kundi H

4 v 2, Port Elizabeth

1 v 3, Ellis Park

Jumanne, Juni 22

Kundi A

2 v 3, Rustenburg

4 v 1, Bloemfontein

Kundi B

2 v 3, Durban

4 v 1, Polokwane

Jumatano, Juni 23

Kundi C

4 v 1, Port Elizabeth

2 v 3, Pretoria

Kundi D

2 v 3, Nelspruit

4 v 1, Soccer City

Alhamisi, Juni 24

Kundi F

4 v 1, Ellis Park

2 v 3, Polokwane

Kundi E

2 v 3, Rustenburg

4 v 1, Cape Town

Ijumaa, Juni 25

Group G

4 v 1, Durban

2 v 3, Nelspruit

Kundi H

2 v 3, Bloemfontein

4 v 1, Pretoria

- -

Mtoano:

Timu 16 bora (Juni 26 hadi 29)

Robo Fainali (Julai 2 na 3)

Nusu Fainali (6 na 7)

Mshindi wa Tatu (Julai 10)

Fainali (Julai 11)


 


Wanandoa wa–gate crash mnuso wa Obama

Enzi zile bwana, minuso ilikuwa inafuatiliwa kwa nguvu zote, iwe umealikwa au hujaalikwa. Ni bora u–gate crash lakini uwe ndani ya nyumba kuliko kuona aibu ukakosa mnuso wa nguvu. Lakini enzi hizo ilikuwa ni minuso ya majumbani.
Marekani yamezuka ma–gate crashers ya aina yake, yamegaye crash mnuso wa Ikulu. Hawa ni wanandoa wawili kutoka Virginia, Michaele na Tareq Salashi ambao Jumanne walifanikiwa kujipenyeza hadi dhifa ya taifa wakati Barack Obama alipomuandalia waziri mkuu wa India chakula cha jioni.
Msemaji wa Ikulu ameeleza kuwa pamoja na wanandoa hao kumudu ku–gate crash mnuso huo, usalama wa Obama haukutikiswa kwa kuwa taratibu zote za ukaguzi wa mlangoni zilifanyika ingawa Salashi na mkewe walipita hapo hapo bila ya kadi.

 

Mambo mengine yanaonekana magumu, lakini yanawezekana. Hapa ni katika kilele cha Mlima Kenya. Waandishi kutoka Kenya, Uganda na Tanzania walijitolea kwenda kupanda mlima huo ambao ni mgumu sana kuupanda kwa ajili ya kusaidia zaidi ya watu milioni 10 waliokuwa wakikabiliwa na njaa. Hili pia linawezekana hapa Tanzania kama kuna mikakati ya ukweli na kama tutaambiana ukweli kuwa wenzetu wako taaban na msaada unahitajika

 


 

Kivazi cha Bi Obama

Bi Obama amekuwa akizingua ulimwengu wa fashion na vivazi vyake vikali lakini vilivyobuniwa na wabunifu ambao si maarufu sana. Wiki hii aliibuka na kivazi hiki kilichobuniwa na Mhindi ambaye sasa amekuwa gumzo

Tuesday, January 15, 2008

 

Kakobe umtoa mpya, lakini hakuweka bayana

Katika moja ya kauli ambazo zimeshangaza wengi tangu kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi wa urais na wabunge nchini Kenya. Ni kweli kuwa wana harakati wote wangependa kusikia kuwa mtu yeyote aliye katika ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati analaani matokeo hayo kuwa Bwana Mwai Kibaki ameiba kura.
Lakini Askofu Kakobe aliibuka na jipya aliposema kuwa anampongeza Kibaki kwa kumshinda Raila Odinga. Ameeleza mengi ikiwa ni pamoja na kumshauri Rais Jakaya Kikwete kutangaza kuitambua serikali ya Kibaki mapema na pia kuwalaumu Watanzania kuwa ni watu wasio wa kweli kwa kushindwa kusema ukweli kuhusu hisia zao.
Lakini Askofu Kakobe hakueleza bayana nini hasa kimemsukuma kutangaza kumuunga mkono Kibaki na kile ambacho pengine anaona kuwa kimemzuia Kikwete kutangaza kumuunga mkono.
Wakati wa mchakato wa kuelekea uchaguzi wa Kenya, Odinga alifanya kosa moja kubwa ambalo ni rafu katika siasa, kuingia katika makubaliano na dini moja na kuacha nyingine zikiwa hazijui mustakabali wao baada ya Odinga kuingia madarakani.
Aliingia makubaliano na Waislamu, na ingawa hatujui kwa undani makubaliano hayo yalikuwa katika maeneo gani, kilichojitokeza dhahiri ni Wakenya waliokimbilia kanisani kuchomwa moto wakiwa hai.
Hadi leo Odinga hajazungumzia hilo na Askofu Kakobe kama kiongozi wa roho za waumini wa Kikristo asingeweza kumuunga mkono mtu aliyeingia makubaliano hayo ambayo baada ya matokeo hayo ya kushangaza kundi la Wakristo wapatao 40 kuchomwa moto wakiwa hai.
Hapa tueleweje?
Ni lazima Askofu Kakobe ampongeze Kibaki!

Tuesday, November 13, 2007

 

Eti Kamati ya Bayser inaadhibu kama Fifa/Caf?

Eti kamati ya Bayser inaadhibu kama Fifa, CAF!

Na Angetile Osiah
ZINEDINE Zidane na Marco Materrazi waliitwa na Shirikisho la Kimataifa la Soka (Fifa) kwenda kujibu shtaka lao lililotokana na sakata lililotokea katika mechi ya fainali ya Kombe la Dunia.
Roy Keane aliitwa na Chama cha Soka cha England (FA) kujibu tuhuma za kutaka kuvuruga mchezo wa soka wakati alipoandika kitabu chake cha maisha ya soka, akiwa ameeleza kwenye kitabu hicho kuwa alimchezea rafu kwa makusudi mchezaji wa timu pinzani.
Na Dean Saunders, mshambuliaji wa zamani wa Liverpool na Aston Villa, alifungua kesi mahakamani akitaka alipwe fidia baada ya kuchezewa rafu ya makusudi iliyokatisha soka lake alilokuwa akilitegemea kwa maisha yake.
Na wachezaji sita wa Arsenal na wawili wa Manchester waliitwa kujieleza mbekle ya FA kutokana na vurugu zilizotokea katika mechi yao ya Ligi Kuu na waliadhibiwa kwa kufungiwa kucheza mechi na kupigwa faini sambamba na klabu zao.
Hayo ni mazingira tofauti yanayotokea kwenye soka na ambayo yanafanyiwa uamuzi tofauti kutoka katika vyombo tofauti. Hiyo ni kujaribu kuelezea kuwa sheria za soka zinatakiwa kuendana na hali na mazingira ya sehemu zinapotumika na si eti kufuata kile Fifa na Shirikisho la Soka la Afrika (CAF) linachoamua.
Msingi wa hoja zangu za leo ni adhabu mfululizo ambazo zimekuwa zikitolewa na Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Soka (TFF) dhidi ya wachezaji, waamuzi na viongozi bila ya kuwapa nafasi ya kujitetea.
Haruna Moshi alifungiwa mechi sita, Athuman Iddi miezi mitatu, Bernard Mwalala mechi sita, na wengine wengi, wakiwemo waamuzi ambao wameondolewa kabisa kwenye orodha ya waamuzi wa Ligi Kuu.
Ni kweli kwamba TFF imepania kupambana na vitendo vya utovu wa nidhamu ambavyo kwa kiasi kikubwa vimekuwa vikichangia sana kutoendelea kwa soka letu. Lakini inaonekana kuwa mkakati huo unatafsiriwa vibaya na watendaji, na hasa Kamati ya Mashindano, ambayo imetumia mwanya huo kuwabandika virungu wachezaji, viongozi na waamuzi bila ya kuwasikiliza.
Wiki hii tulijaribu kupata ufafanuzi kutoka kwa mwenyekiti wa kamati hiyo, Jamal Bayser, ambaye alijibu kifupi tu hawawezi kuwaita watuhumiwa kwa sababu wanachofuata ni taarifa ya refa na kamisaa tu.
Ni kweli kuwa mwamuzi wa mwisho katika soka ni refa, lakini inapotokea matatizo ambayo ni nje ya sheria zake, basi ni lazima wahusika waitwe kutoa ushahidi.
Kwa mfano, kamati haiwezi kubatilisha uamuzi wa kumuonyesha kadi nyekundu mchezaji kwa kuwa hilo hutokea ndani ya dakika tisini, ingawa kwa wenzetu hilo sasa linawezekana baada ya kamati ya nidhamu kuangalia upya mkanda wa video na inapobaini kadi haikuwa halali inaifuta.
Lakini kwa kuwa teknolojia yetu bado iko chini, tutaendelea kuheshimu maamuzi ya refa kama ambavyo Fifa na CAF inaheshimu kutokana na kusita kuanza kutumia teknolojia zaidi ili ubinadamu uendelee kuwepo kwenye soka, yaani makosa ya mwamuzi ni sehemu ya ubinadamu ambao unatakiwa kuheshimiwa mchezoni.
Lakini inapotokea katika taarifa yake, refa anasema alitishiwa na mchezaji, basi madai yake ni lazima yafanyiwe kazi ili ukweli uonekane uko wapi. Ronaldo alishtakiwa kwa kumtukana refa, lakini alipoitwa alikiri kutumia maneno ambayo kwa Kireno ni matusi, lakini akajieleza kuwa hutumia maneno hayo kujijutia na hivyo adhabu yake ikawa ndogo.
Kama asingeitwa, FA isingefikiria kumpa adhabu kama hiyo. Leo hii, Roy Keane ameshtakiwa kwa kosa la kuwaghasi waamuzi wakati wa mechi, lakini na yeye ameripoti FA kuwa mwamuzi aliyechezesha pambano hilo alimtukana. Bila ya Keane kupata nafasi hiyo ya kujieleza, ingefahamika vipi kuwa kumbe alitukanwa.
Hatuwezi kung'ang'ania kuwa refa ni mtu safi anayeweza kusema ukweli bila ya kuweka chumvi kwa nia ya kujilinda au kunufaisha upande mmoja.
Kama kibendera alikataa bao ambalo lilifungwa kutokana na mpira wa kurusha na refa akalikubali eti kwa sababu mchezaji aliotea, lazima mfungaji atajikuta akipanda hasira haraka kwa kuuliza ni refa gani anayeweza kukubali goli la aina hiyo. Ndiyo yaliyomkuta Mwalala.
Unapomuadhibu refa huyo kwa kufanya uamuzi huo wa ajabu, unamuweka wapi mchezaji aliyefanya kosa kutokana na kupandishwa hasira na tukio hilo. Mwite ajieleze ndipo ufikirie adhabu ambayo anastahili kulingana na jinsi alivyochokozwa hadi akatenda kosa na ndio maana kuna makosa ya mauaji na mauaji ya kukusudia ambayo adhabu zake hutofautiana kulingana na mazingira.
Kimsingi, kama Bayser anasema hivyo, maana yake hata hiyo kamati yake kukutana haina maana kwa kuwa tayari adhabu zipo kulingana na kosa lililosemwa na refa. Kinachotakiwa hapo ni kutangaza tu adhabu bila ya kuitisha kikao.
Nachotaka kueleza hapa ni kwamba Tanzania ni nchi ambayo ina utamaduni wake na ina njia zake za kupambana na matatizo yanayokwamisha maendeleo ya soka, na Fifa na CAF zinatoa tu mwongozo wa jinsi ya kushughulikia matatizo hayo bila ya kwenda nje ya kanuni na sheria zake.
Kwa hiyo, TFF na hasa hiyo kamati ya Bayser, haina budi kuandaa taratibu na kanuni za kuadhibu wachezaji kwa kutumia mazingira yetu. Adhabu zinazotolewa sasa hazitaweza kusaidia kukomesha utovu wa nidhamu kama walengwa wataona waliadhibiwa bila ya kutumia haki au waliadhibiwa bila ya masuala yao kuzingatiwa, yaani jinsi kosa lilivyotokea.
Adhabu zitakuwa na maana tu kama wahusika watashiriki katika sehemu fulani ya mchakato wa kutoa uamuzi na hapo ndipo wataweza kujua kuwa masuala yao yalizingatiwa kwa kiasi fulani hata kama wanajua kuwa ni kweli walifanya makosa.
Kutumia mfumo wa Fifa na CAF ni kujidanganya kwa sababu si rahisi kwa vyombo hivyo viwili kumuita mchezaji kama Athuman Iddi aende kujitetea Fifa au CAF kwa kosa alilolifanya nje ya uwanja wakati wa mechi za vyombo hivyo kwa kuwa itakuwa ni vurugu.
Lakini chama cha nchi ni lazima kifanye hivyo kwa kuwa gharama zinakuwa ndogo kulinganisha na zile za kwenda Cairo au Zurich ambako vyombo hivyo vinashughulikia si matatizo ya nchi au mchezaji mmoja, bali karibu nchi 200 kote duniani.
Kwa hiyo, Bayser na kamati yake wasijaribu kukwepa masuala ya msingi kwa kusingizia eti kufuata mfumo wa Fifa na CAF. Waangalia mazingira ya nchi yetu na nini hasa kinahitajika katika kufanikisha mkakati wa TFF wa kupambana na utovu wa nidhamu.


Angetile Osiah
0754 887 222

 

Watanzania Walio Katika 50-Bora ya Riadha Duniani

Wa-Tz walio katika 50 Bora katika riadha duniani

HALF-MARATHON
1. Fabian Joseph Naasi, 24/12/1985
Race: Roterdam Half-Marathon,7th, (01:00:13) 9/9/2007

2. Dickson Marwa Mkami 9/3/1982
Race: Udine Half-Marathon, 8th, (1:00:24) 14/10/2007

3.John Yuda Msuri 9/6/1979
Race: Ras Al Khaim Half Marathon, 6th, (1:00:39) 9/2/2007

4. Andrew Chopa
Race: Vitry-sur-Sienne Half Marathon, 3rd, (1:01:40) 1/4/2007

5. Martin Hhaway Sulle, 28/12/1982
Race: Ras Al Khaim, 13th, (1:01:55) 9/2/2007

6. Samwel Kwaang, 30/11/1985
Race: Udine Half-Marathon, 25th, (01:01:58) 14/10/2007

7. Mohamed Ikoki Msandeki, 3/12/1985
Race: Muscat Half Marathon, 3rd, (01:02:23) 2/2/2007

8. Damian Paul Chopa, 28/11/1986
Race: Saint Dennis Half-Marathon, 4th, (01:02:42) 4/11/2007

9. Patrick Nyangero, 2/5/1986
Race: Gold Coast Half-Marathon,1st, (01:03:00) 1/7/2007


MARATHON

1. Samson Ramadhan, 25/12/1982
Race: Otsu Marathon 1st, (02:10:43) 4/3/2007

2.Mohamed Ikoki Msandeki
Race: Istanbul Marathon, 8th (

3.Lucian Disdery Ilombo, 1979
Race: Warszawa 4th (02:14:15), 23/9/2007

4. Getuli Bayo, 7/6/1980
Race: Wien Marathon, 10th (02:14:17), 29/9/2007

5. Andrea Sambu Sipe, 5/10/1972
Race: Beograd Marathon (02:14:52), 21/10/2007

6.Andrew Silvini, 8/7/1981
Race: Beograd Marathon, 5th, (02:14:56), 21/10/2007

7. Dhako Hana Naftali, 13/9/1983
Race: Beijing Marathon, 13th, (02:16:18) 21/10/07

8.Michael Tluway Mislay, 11/7/1977
Race: Sao Paolo Marathon, 2nd, (02:16:27), 3/6/2007

9. Patrick Nyangero, 2/5/1986
Race: Chunchon, 4th, (02:16:51), 28/10/2007

10,000m

1.Dickson Marwa Mkami, 9/3/1982
Race: Hengelo, 6th, (27:38:58) 26/5/2007

Monday, October 15, 2007

 

Wanaopinga, wajibu hoja za Madega

Na Angetile Osiah
KUNA kila dalili kuwa wakati wa kutotumia busara kuamua mambo umewadia kwa wanachama wa klabu kongwe ya Yanga kama ilivyokuwa mwaka 1994 wakati suala la kampuni lilipoibuka baada ya wafadhili watano kuachia ngazi katika jitihada za kushinikiza katibu wa wakati huo, George Mpondela aachie ngazi.

Ilikuwa ni kipindi kigumu kwa uongozi wa Mpondela, ambaye wakati huo alionyesha msimamo mkali uliofanya apachikwe jina la 'Castro' kutokana na kutokubali kunyenyekea wafadhili hao na kuwaruhusu wawakalie viongozi mabegani.

Wale waliopingana naye hawakutaka kutumia akili na busara zao, na badala yake waling'ang'ania sentensi moja tu kuwa "mpira wa sasa bila ya fedha, hauwezekani" hivyo lazima Mpondela na kundi lake wasalimu amri.

Lakini Mpondela aliungwa mkono na wengi waliojitokeza kupinga vitendo vya wafadhili hao, wajkiongozwa na Marehemu Abbas Gulamali, kumuwekea vikwazo ili ashindwe kuiongoza Yanga na umuhimu wao uonekane ili warejeshwe.

Ilifikia wakati wanachama hao walioweka kando busara zao walidiriki kumbeba Gulamali kumrejesha klabuni kwa nguvu, lakini kundi lililomuunga mkono Mpondela lilikuwa kubwa zaidi na hivyo kufanikiwa kuendelea kushika klabu.

Hujuma, ambazo kwa kawaida huwa hazijipenyezi kwenye timu kila inapotokea mgogoro kwenye klabu ya Yanga, ziliingia kwa kiasi fulani na Yanga ikapoteza mechi moja kabla ya timu kutekwa na wafadhili hao, lakini iliporejea uwanjani ikiwa imehudumiwa kila kitu na wafadhili, ilikung'utwa mabao 3-0 na Sigara kwenye Uwanja wa Taifa.

Ilidhihirika kuwa kuwepo kwa wafadhili hakumaanishi matokeo mazuri uwanjani na timu ikarejeshwa kwa Mpondela na ni wakati wa sakata hilo, Yanga ikawa tishio na kama si 'gundu' ingeweza kufika mbali Afrika, ikiwa na majina kama Constatine Kimanda, Ngandou Ramadhan, Shaaban Nonda, Method Mogella, Steven Nyenge, Mohamed Hussein 'Mmachinga', Maalim Saleh, Anwar Awadh na wengine wakongwe kwa chipukizi na timu ilikuwa ikifundishwa na Mcongo, Tambwe Leya baada ya Charles Boniface kuiongoza kwa mafanikio mwaka uliokuwa umetangulia.

Majina hayo makubwa yalikuwa yamesajiliwa na wafadhili hao, lakini wakataka kuwakalia viongozi mabegani, baadhi ya wafadhili wakitaka kuchapisha kadi za wanachama zenye picha zao, wengine wakiingilia utendaji wa shughuli za kila siku, wengine wakidiriki hata kusema kuwa timu ililazimisha sare Dodoma baada ya refa kupewa fedha ili aongeze muda, kitu kilichomaanisha dharau kwa kocha na wachezaji.

Vituko vilikuwa vingi, kiasi kwamba kundi lililokerwa na ufadhili hilo lilijitokeza na kumuunga mkono Mpondela.
Hali haionyeshi kuwa na mabadiliko sana. Wakati ule wafadhili ndio waliokuwa wakipinga wazo la kampuni na kuwapa fedha wale waliopiga kelele kuwa Yanga ijitegemee. Lakini safari hii ni tofauti ya kimtazamo tu.

Hakuna Yanga Asili wala Kampuni, lakini tofauti iliyopo ni ile ya jinsi ya kutekeleza wazo hilo.Vinara wa makundi hayo wamebadilika, lakini wale wanaosukuma kuwepo kwa hali hiyo ni wale wale waliokuwepo wakati wa mgogoro wa mwaka 1994. Angalia televisheni au soma magazeti utaona walio katikati ya mgogoro huo ni wale wale waliosumbua mwaka 1994.


Hali ya kufanana pia ipo kwenye timu, yaani idadi kubwa ya wachezaji imesajiliwa na mfadhili, na kama ilivyokuwa kwa akina Ndonda, Ngandou, Kimanda na Method, ambaye alinunuliwa toka Simba, safari hii wapo Laurent Kabanda, Bernard Mwalala, Maurice Sunguti, Aime Lukunku na Athuman Iddi, ambaye alichukuliwa Simba.

Kama nilivyosema tofauti ni mtazamo au njia ya utekelezwaji wa jinsi ya kuhamisha timu kutoka kwenye uongozi wa klabu kwenda kwenye uongozi wa kampuni, ambao nahisi haupo.

Mwenyekiti Imani Madega alijitokeza mapema wiki hii na kueleza jinsi alivyotofautiana kimtazamo na mfadhili, ambaye pia ni mdhamini wa Yanga, Yusuf Manji, katika zoezi zima la utekelezwaji wa suala hilo. Ameeleza jinsi klabu inavyokosa uwakilishi wa kutosha kwenye kampuni licha ya kuwepo kwa maneno kuwa ndiyon itakayomiliki asilimia 51 za hisa.

Ameeleza udhaifu wa katiba na jinsi walivyowasiliana na Manji kuhusu kuzirekebisha kasoro hizo kwa njia ya kuunda kamati ndogo ili marekebisho hayo yafanyike katika muda usiopungua miezi mitatu, na ameeleza jinsi klabu itakavyokuwa na hisa saba tu zenye thamani ya Sh 7,000.

Pia amechambua udhaifu wa rasimu ya muafaka, ambayo imejumuishwa kwenye katiba mpya na kuwa sehemu ya katiba na jinsi alivyowasiliana na Manji juu ya njia za kuondoa udhaifu huo na haja ya kuwepo uwazi katika suala zima la utekelezwaji wa mpango huo.

Pia ameeleza jinsi ilivyokuwa tatizo kutekeleza zoezi la kusajili wanachama katika muda wa siku nane tangu Manji atoe barua ya kukubali kutoa Sh milioni 10 alizoombwa kwa ajili ya zoezi hilo, akisema kuwa uongozi ulitaka kuangalia jinsi ya kulifanya zoezi hilo ili fedha zitakazotolewa na wanachama kulipia ada ziingie kwenye mifuko sahihi ya klabu.

Hata sharti la kukabidhi timu siku moja tu baada ya uchaguzi, nalo lilikuwa na mashaka, kama alivyoeleza Madega.
Na la mwisho ambalo hakulisema lakini ambalo linazungumzwa ni jinsi Manji anavyoshupalia suala la timu kuhamishiwa kwenye kampuni bila ya kulishupalia kundi la kampuni kukamilisha taratibu za usajili wa kampuni ili iweze kuwa tayari kukabidhiwa timu.

Ni kweli kuwa kampuni bado haijakamilisha usajili tangu ilipokubaliwa kuwa muundo wa kampuni ubadilike tofauti na ile iliyosajiliwa awali wakati Manji hajaingia kusuluhisha makundi yaliyokuwa yanapingana.

Nilidhani kuwa hoja hizo za Madega zingezua mjadala na wale wanaompinga wangefanya jitihada za kuzijibu ili waonyeshe kuwa amekosea, lakini badala yake nilishangazwa kuona taarifa ya viongozi wenzake ikimkana Madega bila ya kujibu hata hoja moja alizozitoa.
Taarifa hiyo ya juzi inaonyesha kumnyenyekea zaidi Manji na kukwepa kabisa kuzungumzia kasoro ambazo Madega alizionyesha katika kutekeleza utashi wa Manji wa kutaka timu ikabidhiwe kwa kampuni na klabu kuongeza wanachama ili ijenge mtaji wake.
Kutozungumzia hoja za Madega ni kuipumzisha akili kufanya mambo ambayo yangeisaidia klabu. Binafsi naona hoja za Madega zina nguvu na wakati huu wanachama wanapoibuka kumuomba msamaha Manji kwa kauli za Madega na kumshutumu mwenyekiti wao, wangeonyesha ni kwa vipi hoja za Madega si za msingi na zoezi la kuikabidhi timu litatekelezwaji bila ya kuzingatia hoja hizo.
Ni kweli Yanga inamuhitaji Manji kama inavyohitaji wadhamini wengine, lakini inapoonekana kuna matatizo ni vizuri yachunguzwe na kuwekwa sawa ili mambo yaende bila ya matatizo.
Tujibu hoja za Madega na si kurushiana matusi na kuviziana.

This page is powered by Blogger. Isn't yours?