Friday, November 27, 2009

 

Sita wateuliwa kusimamia uchaguzi Yanga

Sosthenes Nyoni

UONGOZI wa klabu ya Yanga umetangaza majina ya wajumbe watano watakaounda kamati itakayosimamia uchaguzi mkuu wa klabu hiyo uliopangwa kufanyika Januari 3 mwakani.

Mwenyekiti wa Yanga, Imani Madega alisema kuwa kamati hiyo itafanya kazin kwa kushirikiana na Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Soka Tanzania(TFF).

Madega aliwataja watu wanaunda kamati hiyo kuwa ni pamoja na Jaji John Mkwawa ambaye atakuwa mwenyekiti wa kamati hiyo, Ridhiwan Kikwete ambaye ni mtoto wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Angetile Osiah , Philemon Ntahilaja na mwenyekiti wa zamani wa matawi ya Yanga asili, Yusuph Mzimba.

Alisema kuwa uteuzi huo umezingatia katiba ya klabu hiyo iliyofanyiwa marekebisho Agosti 8 2006 iliyotaka kamati ya uchaguzi kuwa na watu wasiopungua watano na wasiozidi saba.

"Uteuzi wa majina haya umezingatia katiba ya Yanga iliyofanyiwa marekebisho Agosti 8 2006 ambapo inaelekeza kuwa kamati ya uchaguzi inatakiwa kuwa na watu wasiopungua watano na wasiozidi saba,"alisema Madega.

Aliongeza kuwa uongozi wa klabu hiyo utakutana na wajumbe hao ili kuelezana majukumu yanayotakiwa kufanywa wakati wa zoezi hiyo la uchaguzi.

Madega, pia aliwataka wanachama wa klabu hiyo kutumia haki yao ya kuwachagua viongozi wanaowataka kwa kuhakikisha wanalipa ada za uanachama wao ili wawe wanachama hai na wenye sifa za kushiriki uchaguzi.

"Haki mojawapo ya mwanachama ni kuchagua kiongozi anayemtaka, hivyo natoa wito kwa wanachama ambao hawajamaliza ada za uanachama wao walipe ili wawe na sifa ya kushiriki katika uchaguzi,"alisema Madega.

Thursday, November 26, 2009

 
CAF reminds National Associations of Inter-clubs entry deadline
11-25-2009
CAF reminds National Associations of  Inter-clubs entry deadline
Zoom
The Confederation of African Football is reminding all National Associations to submit the list of their representatives for the CAF Inter-clubs competitions, Orange CAF Champions league and Orange Confederation Cup, before 30th of November 2009.
According to Article 2, paragraph 2 of CAF Inter-clubs regulations, the application must reach CAF by mail, fax or e-mail not later than 30th of November of the year preceding the Competition.

 

Tanzanian Striker Joseph Kaniki Signs for Swedish Premier Side

Former Tanzanian Simba striker Joseph Kaniki has finally signed a two-year contract with Gefle IF of Sweden for the Premier Division League.

Ndumbalo Soccer Agency managing director Damas Ndumbalo told The Citizen that striker passed his trials in Sweden. Kaniki will join fellow Tanzanian Haruna Moshi who secured a contract with the Swedish club recently.

"The duo flew to Sweden for trials with Gefle earlier this month and both have passed their trials," he said.

Kaniki, who was plying his trades at Rayon Sports of Rwanda, finished his contract before moving to Sweden. Ndumbaro said they had already applied for his International Transfer Certificate (ITC) from Rwanda's soccer body, FERWAFA.

Simba allowed Moshi to fly out to Sweden only three days before clashing with their archrivals, Young Africans in the high flier Dar Es Salaam.


 

Ratiba ya fainali za Kombe la Dunia 2010

Pilikapilika za Kombe la Dunia ndio zimeshaanza na hii hapa ni ratiba ya fainali hizo kabla ya kuchomekwa majina ya nchi.

Ijumaa, Juni 11

Kundi A

Team 1 v Team 2, Johannesburg (Soccer City)

Team 3 v Team 4, Cape Town

Saturday, June 12

Kundi B

1 v 2, Johannesburg (Ellis Park)

3 v 4, Port Elizabeth

Group C

1 v 2, Rustenburg

Jumapili, Juni 13

Kundi C

3 v 4, Polokwane

Group D

1 v 2, Durban

3 v 4, Pretoria

Jumatatu, Juni 14

Kundi E

1 v 2, Soccer City

3 v 4, Bloemfontein

Group F

1 v 2, Cape Town

Jumanne, Juni 15

Group F

3 v 4, Rustenburg

Kundi G

3 v 4, Port Elizabeth

1 v 2, Ellis Park

Jumatano, Juni 16

Kundi H

3 v 4, Nelspruit

1 v 2, Durban

Group A

1 v 3, Pretoria

Alhamisi, Juni 17

Kundi A

4 v 2, Polokwane

Group B

4 v 2, Bloemfontein

1 v 3, Soccer City

Ijumaa, Juni 18

Kundi D

1 v 3, Port Elizabeth

Kundi C

4 v 2, Ellis Park

1 v 3, Cape Town

Jumamosi, Juni 19

Kundi D

4 v 2, Rustenburg

Kundi E

1 v 3, Durban

4 v 2, Pretoria

Jumapili, Juni 20

Kundi F

4 v 2, Bloemfontein

1 v 3, Nelspruit

Kundi G

1 v 3, Soccer City

Jumatatu, Juni 21

Kundi G

4 v 2, Cape Town

Kundi H

4 v 2, Port Elizabeth

1 v 3, Ellis Park

Jumanne, Juni 22

Kundi A

2 v 3, Rustenburg

4 v 1, Bloemfontein

Kundi B

2 v 3, Durban

4 v 1, Polokwane

Jumatano, Juni 23

Kundi C

4 v 1, Port Elizabeth

2 v 3, Pretoria

Kundi D

2 v 3, Nelspruit

4 v 1, Soccer City

Alhamisi, Juni 24

Kundi F

4 v 1, Ellis Park

2 v 3, Polokwane

Kundi E

2 v 3, Rustenburg

4 v 1, Cape Town

Ijumaa, Juni 25

Group G

4 v 1, Durban

2 v 3, Nelspruit

Kundi H

2 v 3, Bloemfontein

4 v 1, Pretoria

- -

Mtoano:

Timu 16 bora (Juni 26 hadi 29)

Robo Fainali (Julai 2 na 3)

Nusu Fainali (6 na 7)

Mshindi wa Tatu (Julai 10)

Fainali (Julai 11)


 


Wanandoa wa–gate crash mnuso wa Obama

Enzi zile bwana, minuso ilikuwa inafuatiliwa kwa nguvu zote, iwe umealikwa au hujaalikwa. Ni bora u–gate crash lakini uwe ndani ya nyumba kuliko kuona aibu ukakosa mnuso wa nguvu. Lakini enzi hizo ilikuwa ni minuso ya majumbani.
Marekani yamezuka ma–gate crashers ya aina yake, yamegaye crash mnuso wa Ikulu. Hawa ni wanandoa wawili kutoka Virginia, Michaele na Tareq Salashi ambao Jumanne walifanikiwa kujipenyeza hadi dhifa ya taifa wakati Barack Obama alipomuandalia waziri mkuu wa India chakula cha jioni.
Msemaji wa Ikulu ameeleza kuwa pamoja na wanandoa hao kumudu ku–gate crash mnuso huo, usalama wa Obama haukutikiswa kwa kuwa taratibu zote za ukaguzi wa mlangoni zilifanyika ingawa Salashi na mkewe walipita hapo hapo bila ya kadi.

 

Mambo mengine yanaonekana magumu, lakini yanawezekana. Hapa ni katika kilele cha Mlima Kenya. Waandishi kutoka Kenya, Uganda na Tanzania walijitolea kwenda kupanda mlima huo ambao ni mgumu sana kuupanda kwa ajili ya kusaidia zaidi ya watu milioni 10 waliokuwa wakikabiliwa na njaa. Hili pia linawezekana hapa Tanzania kama kuna mikakati ya ukweli na kama tutaambiana ukweli kuwa wenzetu wako taaban na msaada unahitajika

 


 

Kivazi cha Bi Obama

Bi Obama amekuwa akizingua ulimwengu wa fashion na vivazi vyake vikali lakini vilivyobuniwa na wabunifu ambao si maarufu sana. Wiki hii aliibuka na kivazi hiki kilichobuniwa na Mhindi ambaye sasa amekuwa gumzo

This page is powered by Blogger. Isn't yours?